vitabu nivipendavyo

  • where have all the leaders gone,uongozi wetu na hatma ya Taifa letu,makuhadi wa soko huria

VIJANA TUAMKE

tunataka kuona vijana wasomi wanaoweza kuhoji mfumo wowote wa kisiasa na kiuchumi unaokandamiza jamii,siyo vijana akina 'ndiyo bwana'wanafiki,wenye nidhamu ya woga na wabeba vipeperushi vya mafisadi.kama vijana wasomi,tusipofanya hivyo,JAMII ITAOTA KUTU,ITASAGIKA NA KUTEKETEA

Monday, September 17, 2012

KIJANA KUWA TAJILI WA MAWAZO NA SIYO KUIGA MAISHA NA TAMADUNI

Itakua vigumu kumshawishi mtu aliyevaa sare za kijeshi kua ni raia.Kwa maana hiyo malaya atavaa nguo zinazofanana na shughuri yake,kwa mavazi mwanadam anajulisha marazi yake.Mtakatifu atajulikana kwa moyo wake na mavazi yake.Kwa maana hii usemi kua MUNGU huangalia roho tu umepotoshwa ili mwanadamu apatekunajisi mwili wake,maandiko yanaposema kuwa MUNGU huangalia roho yana maana kwamba kila jambo jema chanzo chake ni rohoni.
                              "MUNGU akaona kila kitu alichokifanya,natazama ni chema sana"
                                 Mwanzo 1;31
MUNGU akumuumba mwafrika peke yake akiwa mwema sana,bali watu wote kwa jinsi yao,kwa faidayao kutokana na mazingira alimwowaweka,na kwa ajili ya utukufu wake.Kwa maana hii mwafrika si mweusi kwa bahati mbaya . Kwa maana hii mzungu hawezi kuheshimika kwa kujipaka masizi ili awe mweusi na hivyo hivyo kujikwangua kujikwangua kwa mwafrika hakumfanyi kuwa mzungu.Kinyume chake,KUNAMDHALILISHA.Madhumuni ya msingi ya kuvaa ni kufunika mwili .Mavazi ya kukosesha ni machukizo kwa MUNGU.Hekima katika mavazi ni muhimu sana.Kama hutakua shahidi wangu siku hizi kuna wimbi la tabia za ajabu ajabu ktk jamii yetu
1/.Vipodozi na madawa ya kuchoma nywele vina madhara makubwa,ila tunavipenda
2/.Ulevi na utumiaji wa sigara kwa vijana wa kitanzania umeongezeka,mpaka wanawake nao days wanatupia sigara na ni walevi
3/.Mavazi ya vishawishi kwa dada zetu yamekubalika tayari wanavaa nguo wanaachia kifua kionekane,mapaja kuonekana na yenye kubana na kuonesha ramani ya mwili wako wote.
4/.Kusahau hali za maisha na tuliko toka kwa vijana wa vyuoni tanzania imekua fasheni mtu anasahau kua familia yake imeuza shamba ili yeye asome lakini watu tunajisahau.
MWISHO namnukuu dada yangu Riyama Ally aliniandikia hivi siku moja "Naamini kuwa ukijitambua utaweza kumtambua muumba wako,utaweza kutambua majukumu yako wazazi wako dini yako kwa kufanya ibada na kuwatambua wanaokuzunguka kwa namna ya kuwaheshimu na kujiheshimu.Duniani kote hakuna star zaidi ya MUNGU.Ni mapito tu ambayo kesho hayata kuwa na nafasi mbele za MUNGU.Amal yako njema na ibada ndizo zitakazo kuweka katika pepo na kukuingiza katika ufalme wa MUNGU "
VIJANA TUACHE KUIGA NA KUISHI MAISHA TOFAUTI NA ASILI ZETU.

Monday, September 10, 2012

KICHWA KINA MENGI KIJANA MWENZANGU

Kichwa chako kina ubongo ambao hufanya kazi ya kutoa na kupokea mawimbi ya mawazo yanayotolewa na ubongo wa watu wengine.Ni sehemu pekee ambayo binadamu hupokea na kutunza mawazo au fikra za aina fulani.Maajabu makubwa na ugunduzi ambao binadamu hufanya huanzia katika fikra alizonazo,vilevile utajiri wa binadamu huanzia katika mitazamo yake ya kutumia fikra alizo nazo juu ya maisha yake na mazingira yake yanayomzunguka kwa wakati fulani.Maisha ya binadamu huongozwa na nguvu ya fikra zitokanazo kichwani mwake kwa mfumo wa imani aliyonayo ya maisha yake hapa duniani.MWISHO Kila mwanadamu wa dunia hii anakitu ndani yake kinachoweza kutubadili sisi jinsi tunavyoishi,tunavyocheza na tunavyotenda...............KIJANA TUMIA FIKRA ZAKO KATIKA KUBADILISHA MAISHA YAKO NA JAMII INAYOKUZUNGUA KWA KUWAZA FIKRA SAHIHI KWA MALENGO SAHIHI KWAKO NA JAMII