vitabu nivipendavyo

  • where have all the leaders gone,uongozi wetu na hatma ya Taifa letu,makuhadi wa soko huria

VIJANA TUAMKE

tunataka kuona vijana wasomi wanaoweza kuhoji mfumo wowote wa kisiasa na kiuchumi unaokandamiza jamii,siyo vijana akina 'ndiyo bwana'wanafiki,wenye nidhamu ya woga na wabeba vipeperushi vya mafisadi.kama vijana wasomi,tusipofanya hivyo,JAMII ITAOTA KUTU,ITASAGIKA NA KUTEKETEA

Wednesday, August 24, 2011

kuna usemi usemao ''mtoto ni taifa la kesho''siupingi kwani umekuwa imara tokea enzi za baba wa taifa hayati Mwl.Nyerere,usemi huo ulikuwa ukionekana upo hai,lakipi kwa sasa kuna usemi ''mtoto ni taifa la leo na kesho''nao siupingi kwani umelenga kuwa ndio nguvu ya Taifa sasa cha muhimu ni jinsi gani mtoto huyu anavyo wezeshwa kufikia kuwa taa ya Taifa kwa kumpatia malezi bora na ELIMU BORA,kwa sasa hakuna ubishi wanafunzi tumekumbwa na matokeo hatari kwa maendeleo ya nchi yetu na kiwango cha elimu kimeshuka,sasa tunamrithisha nini mtoto huyu hasa mtoto wa mkulima na masikini ambaye elimu ndio urithi wake pekee,kwani wenye nazo wako salama na familia zao na pesa ya kununua mtihani ipo,SASA WAPI MTOTO MWENZANGU WA MKULIMA NA MASIKINI WA MTANZANIA,AMKA TUPAMBANE KUPATA ELIMU BORA.